ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 17, 2017

MCHEZO WA KUMBUKUMBU YA ISMAIL MWANZA 'KITUO KILICHOMLEA KINASEMA HAKITOKATA TAMAA KUSAKA VIPAJI NA WAKALI WENGINE'

Naibu waziri wa Habari, utamaduni na Michezo Anastazia Wambura akizungumza na malfu ya wanafunzi na wananchi wa mkoa wa Mwanza waliojitokeza katika uwanja wa CCM Kirumba kwenye Tamasha la michezo la kumuenzi mchezaji wa U20 aliyefariki uwanjani mkoani Kagera mjini Bukoba Ismail Halfan, ikiwa ni sehemu ya kuchangisha fedha zitakazo tumika kuifariji familia yake.

Meza kuu.
Ndugu wa karibu waliojitokeza katika uwanja wa CCM Kirumba kwenye Tamasha la michezo la kumuenzi mchezaji wa U20 aliyefariki uwanjani mkoani Kagera mjini Bukoba Ismail Halfan, ikiwa ni sehemu ya kuchangisha fedha zitakazo tumika kuifariji familia yake.

Khalid Bitegeko (kulia) ni Afisa Michezo jiji la Mwanza akiwa na Afisa Michezo wilaya ya Ilemela (kushoto).
Mc Seki shughulini.
Burudani ya utangulizi ilisanukishwa na Dogo Dee.



Dogo Dee part two.
Kwa utulivu wanafunzi toka shule mbalimbali macho kwenye mchezo.
Wanafunzi hawakutaka kuwa nyuma kushiriki siku hii ya kumbukumbu ya mwenzao.



Msanii Sajna aliwakosha wahudhuriaji na kazi zake.
Wanafunzi walionesha vipaji.
Kwa stage...
Macho mbele...
Kiduku kikipata tabu.
ShangwezZZ.

BAADA YA BURUDANI MTANANGE:- NYAMAGANA Vs ILEMELA

Naibu waziri wa Habari, utamaduni na Michezo Anastazia Wambura akikagua wachezaji wa Kombaini ya wanafunzi wa Shule za Ilemela katika uwanja wa CCM Kirumba kwenye Tamasha la michezo la kumuenzi mchezaji wa U20 aliyefariki uwanjani mkoani Kagera mjini Bukoba Ismail Halfan, ikiwa ni sehemu ya kuchangisha fedha zitakazo tumika kuifariji familia yake.
Naibu waziri wa Habari, utamaduni na Michezo Anastazia Wambura akikagua wachezaji wa Kombaini ya wanafunzi wa Shule za Nyamagana katika uwanja wa CCM Kirumba kwenye Tamasha la michezo la kumuenzi mchezaji wa U20 aliyefariki uwanjani mkoani Kagera mjini Bukoba Ismail Halfan, ikiwa ni sehemu ya kuchangisha fedha zitakazo tumika kuifariji familia yake.
Naibu waziri wa Habari, utamaduni na Michezo Anastazia Wambura akitoa neno kwa wachezaji.
 Ilemela wakitoa salamu kwa Nyamagana. 
Ilemela.

Nyamagana.
Bonge la chenga... mchezaji wa Nyamagana akifanya yake.
Licha ya Ilemela na kasi yao mchezoni huku wakitangulia kufunga katika dakika za awali kipindi cha pili Nyamagana walikuja juu na kusawazisha kisha wakaongeza la ushindi. Hivyo hadi dakika 90 ziamalizika Ilemela wanatota 1-2 dhidi ya Nyamagana.
Hatari langoni mwa Nyamagana
Mbaki Mutahaba ambaye ni Mkurugenzi wa The Footbal House (TFH ) kituo kilichomlea marehemu Ismail Halfan akizungumza na Gsengo Blog.
Khalid Bitegeko (kulia) ni Afisa Michezo jiji la Mwanza (kushoto) akizungumza na Gsengo kupitia Jembe Fm.
"Licha ya mchezo huu kuwa kumbukumbu na kumthaminisha mtoto wetu aliyetangulia mbele za haki pia mchezo huu tunaufanya kama maandalizi kwa wanafunzi kuelekea mashindano ya Umiseta na Umishumta yatakayoanza mapema mwezi wa pili na watatu" 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.