ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 19, 2018

PICHA:- JINSI ILIVYOFANA HAFLA YA KUTUNUKU VYETI VYA TUZO ZA MWANAMKE JEMBE 2018.

Mkuu wa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Mhe. Marry Tesha akihutubia kusanyiko la utoaji wa Vyeti vya Tuzo za Mwanamke Jembe zilizoandaliwa na kituo cha redio Jembe Fm kutoka Mwanza, hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki Jembe Beach jijini humo.
Serikali inatambua na kuthamini sana ushirikiano baina yenu na harakati za maendeleo katika Mkoa wetu.  

Ndiyo maana tumekuwa tunatengeneza mazingira mazuri kwa wanawake. Tumekuwa tunatoa mikopo kwa makundi ya wajasiriamali tumewaboreshea vituo Afya ,na mazingira mengine mengi.
Meneja wa Jembe Media Group Fred Kikoti akitoa historia ya kituo na shughuli mbalimbali za kituo kwa jamii tangu uanzishwaji wake.
Wadada makini wa Mwanza ndani ya  kusanyiko.
Sehemu ya wahudhuriaji wa hafla ya Mwanamke Jembe.
Safi.
Tunaimani mchakato huu ulifuata hatua zote stahiki za kumpata Mwanamke Jembe ambaye anawakilisha  WANAWAKE  MAJEMBE wengine kutoka katika mkoa wetu, hii ni hatua nzuri ya kuwainua wanawake hawa ili na wao wafike katika  viwango vinavyohitajika katika soko la sasa la kimapinduzi katika maendeleo.
Kwa umakini wadau wakifuatilia kilichokuwa kikijili wakati huo.
Mkurugenzi wa Shirika la kutetea haki za wanawake na watoto la KIVULINI Bw. Yassin Ally amesema wanawake wengi huangushwa na wanawake wenzao.
Mmoja kati ya wafanyabiashara wenye mafanikio jijini Mwanza Dida Vitenge Wear naye alisimama kutoa neno la shukurani sanjari na kuwasilisha uzoefu alioupata kupitia harakati zake za ujasiliamali.
Team Sega "Mambo ni Motto" nao walishiriki kama wadhamini Mwanamke Jembe 2018.
Aksante sana kwa Lake Zone Tents and Supply kupitia Bi. Rose kwa kuwa sehemu ya wadhamini wa Mwanamke Jembe 2018.
Meneja wa Vipindi kituo cha Redio Jembe Fm Kelvin Michael (Deejay Kflip) akitambulisha safu ya watangazaji wa Jembe Fm (hawapo pichani).
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Mhe. Marry Tesha akimpongeza mshindi wa kwanza Tuzo za Mwanamke Jembe 2018 Bi. Amina Khamisi ambaye amekuwa akiishi na virusi vya ukimwi tangu mwaka 1982 na amekuwa akiwahudumia na kuwapa moyo na darasa la masuala ya afya watu waishio na VVU, ni kupitia tuzo zilizoandaliwa na kituo cha redio Jembe Fm Mwanza, hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki Jembe Beach jijini humo.
Dada huyu (kulia) Deborah Mwambo ni mjasiliamali licha ya kukosa ada akiwa hana wazazi wa kumsaidia aliamua kujishughulisha na kazi za ndani huku akijisomesha leo hii anajivunia mafanikio aliyonayo kwani ameweza kujenga nyumba pia akijitegemea. 
Mkurugenzi wa Shirika la kutetea haki za wanawake na watoto la KIVULINI Bw. Yassin Ally (kulia) akikabidhi Bi. Aisha Mtumwa Cheti cha Tuzo ya Huduma kwa Watoto.
Mkurugenzi wa Club 255 Bi. Siwema (kushoto) akimkabidhi Cheti cha Tuzo za Mwanamke Jembe kipengele cha Michezo iliyokwenda kwa Consolata Lazaro (kulia) ambaye ni mwamuzi wa kike wa Ligi kuu Soka Tanzania Bara kutoka Mwanza. 
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Mhe. Marry Tesha (kulia) akikambidhi cheti cha Shukurani kwa Meneja wa Jembe Media Group Fred Kikoti na hii ni kwa niaba ya kutambua mchango wa Mkurugenzi wake Dr. sebastian Ndege kwa shughuli na harakati za akinamama mkoa wa Mwanza katika hafla ya Tuzo za Mwanamke Jembe zilizofanyika mwishoni mwa wiki.
Mkuu wa Vipindi toka Jembe Fm Radio Kelvin Michael (kushoto) akimkabidhi Cheti cha Shukurani na kutambua mchango wa Mkuu wa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Mhe. Marry Tesha katika hafla ya kukabidhi Tuzo za Mwanamke Jembe zilizofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza.
 Aksante ni neno kubwa sana.
Mkuu wa Vipindi Msaidizi wa Jembe Fm Radio Harith Jaha (kulia) ambaye alikuwa Jaji Mkuu wa mchakato mzima, akifafanua sifa za mshiriki mshindi wa Kwanza Amina Khamisi kabla ya kumkabidhi Tuzo na Cheti katika hafla ya kukabidhi Tuzo za Mwanamke Jembe zilizofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza.
Ilivyokuwa Jiografia ya eneo la tukio.
Mwanamke Jembe.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Marry Tesha akikata keki iliyoandaliwa kama sehemu ya kumbukumbu ya maadhimisho ya Tuzo za Mwanamke Jembe 2018.
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Mhe. Marry Tesha katika picha ya pamoja wadau wafanikishaji kutoka kushoto Meneja wa Jembe Media Group Fred Kikoti, Mratibu wa Mwanamke Jembe 2018 Mansour Jumanne na Mkurugenzi wa Shirika la kutetea haki za wanawake na watoto la KIVULINI Bw. Yassin Ally (kulia)
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Mhe. Marry Tesha katika picha ya pamoja na Ma-Mc wa tuzo sanjari na wadau wa Meza kuu. 
Picha ya pamoja.
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Mhe. Marry Tesha katika picha ya pamoja na washiriki wa Tuzo sanjari na wadau wa Meza kuu.
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Mhe. Marry Tesha katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Jembe Fm Mwanza.

HOTUBA YA MKUU WA  MKOA WA MWANZA  , MHESHIMIWA   JOHN MONGELA  AMBAYO ITASOMWA NA MKUU WA WILAYA NYAMAGANA MAMA MARRY TESHA , KATIKA UTOAJI WA VYETI NA ZAWADI KWENYE KILELE CHA  MWANAMKE  JEMBE  MWANZA , TAREHE 17  MARCH , 2018

Waheshimiwa viongozi wa JEMBE MEDIA GROUP,

Waheshimiwa Wageni Wote toka Ndani na Nje ya Mkoa wa Mwanza;
Waheshimiwa Wanawake Wote Mliopo Hapa;
Mkurugenzi wa Kivulini Bw. Yassin Ally;
Mabibi na Mabwana;
Bwana Yesu Asifiwe : AsalamAleikum
Mwanamke JEMBE Oyeee
Mwanamke Jembe Saaafiiii

Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa afya njema katika siku ya leo, Pia napenda kuwashukuru sana Uongozi wa Jembe Fm kwa kunialika na kunishirikisha kwenye ugawaji wa vyeti kwa akinamama, wadada ambao wamekuwa sehemu ya maendeleo ya jamii yetu, na sehemu ya maendeleo katika mkoa wetu wa Mwanza  yaani (MWANAMKE JEMBE) Kwa kweli ni jambo la furaha na heshima kubwa kwangu kujumuika nanyi kwa tukio hili kubwa na la kihistoria katika Mkoa wetu.

Mwaliko wenu huu kwangu ni uthibitisho mkubwa wa uhusiano mzuri uliopo baina ya JEMBE FM 93.7 MWANZA, Wakina Mama  na Serikali Katika Mkoa wetu.

Uhusiano ambao umekuwa na manufaa makubwa kwa mkoa wetu na watu wake. Uhusiano  ambao umejitafsiri katika umoja, upendo, amani, na mshikamano uliopo baina ya WanaMwanza

Mwanamke Jembe
Ndugu wanawake, Wananchi na Wageni Waalikwa;

Miaka 5 iliyopita, Mkurugenzi wa kituo cha Radio Jembe fm, DR. Sebastian Ndege  alikuja na wazo la kuanzisha kituo cha radio Mkoani Mwanza wazo lake lilifanikiwa na ndipo hapo kituo cha Radio cha Jembe Fm kikaanzishwa katika mkoa wetu wa Mwanza, Kituo hiki kilianzishwa Kwa lengo la kuwa habarisha wana Mwanza, kuburudisha na kuelimisha, Pamoja na yote hayo kituo cha radio Cha jembe FM, kimekuwa sehemu ya msaada kwa wananchi na kimekuwa kiunganishi kati yetu na jamii.

Huo pia ndiyo misingi wa JEMBE fm ambayo imekuwa tegemeo kubwa kwa Wananchi wa MWANZA.

Licha ya kutumia viongozi wetu wa mitaa wakiwemo wenyeviti na mabalozi, katika ufikishaji wa taarifa na elimu kwa wananchi, SISI Serikali Jitihada zetu za kuondoa umasikini, kuboresha huduma za afya na masuala mengine muhimu kwa miaka ya sasa yenye mapinduzi ya teknolojia hutegemea kwa namna kubwa sana uwepo wa vyombo vya habari.

Jitihada za Serikali zinapounganika na zile za vyombo vya habari tunatengeza nguvu kubwa ya kuwaondolea wananchi wetu siyo tu unyonge wa kukosa habari, bali pia kuwapunguzia changamoto za maendeleo zinazowakabili na kusaidia kuinua hali zao za maisha.

Mchango wa Jembe FM katika Mkoa wetu
ndugu Wanawake .

Ninaposema hivyo, natambua mchango wa Jembe FM katika kuhabarisha jamii ya watanzania hususani mkoa wetu wa Mwanza, Mimi ni shahidi, maana nimekuwa nikipata taarifa ya habari kutoka katika kituo hiki cha habari, nimewahi kuwa shuhudia Jembe fm katika Kampeni ya Usalama barabarani ambayo walishiriki bega kwa bega na jeshi letu la Polisi kitengo cha Usalama barabarani.

Nimeshuhudia Jembe Fm wakiwa na kampeni ya kumwinua mtoto (MTOTO JEMBE) Pia hata katika burudani wote tumekuwa tukishuhudia Jembe Fm wa kituletea wasanii kutoka ndani na nje ya Tanzania  kupitia Tamasha lao la kila mwaka la JEMBEKA FESTIVAL, Tuliwahi kuwashudia hata wasanii wa kimataifa, kutoka nchini Marekani akina NEYO na wengine wengi na hata wale wanaotamba hapa nchini  akina Diamond,Maua Sama, Juma Nature, Ruby nakadhalika. Tena mwaka huu tamasha hilo sijaliona sijui kwanini?

JEMBE FM  inatoa habari za kipekee ambazo hazipatikani kwa urahisi katika vituo vingine vya habari.

Ninyi mna vipindi vizuri kama : KAZI NA NGOMA , DRIVE MIX, SEGA LA LEO, MCHAKAMCHAKA, KIKOBA, SPORTS RIPOTI  NK , Hivi tu ni baadhi ya vipindi ambavyo kwetu tunadiriki kusema kuwa mnafanya kazi nzuri.

Kwa upande wa Afya nimekuwa nikiwasikia namna mnavyo hamasisha watu kuwasaidia wenye matatizo ya Afya na saa nyingine kuhamasisha watu kuwachangia ili wafanikishe ndoto zao, Hongereni sana.

Kwa miaka mingi sana wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika kupigania haki zao za msingi na kupigania maendeleo si tu ya jamii inayowazunguka bali hata kwa maendeleo ya taifa na mtu mmoja mmoja, Niwapongeze wanawake wote  wa mkoa wa Mwanza kwa kulifanikisha hilo.

Miaka ya zamani wanawake walikatazwa kujishughulisha na shughuli za uzalishaji na kiuchumi na walikuwa ni watu wa ndani tu, ila tunaishukuru jamii kwa kutambua umuhimu wa wanawake na kuwaruhusu kuingia katika shughuli za uchumi, na uzalishaji mali, na ndio maana leo tunashuhudia idadi kubwa ya wajasiriamali, wafanyabiashara wakubwa, madaktari, wahandisi, waandishi wa habari, walimu na wanajamii wakutosha ndani ya mkoa wetu.

Mwanamke Jembe mlianza rasmi mwaka Jana, mwaka huu naona mmeboresha zaidi lakini tunawaomba mwakani mwanamke  JEMBE iwe maradufu zaidi ya hii ya leo, kuwe na zawadi za kutosha, wadhamini wajitokeze kuwasapoti na sisi Serikali tunawaahidi hatutawaangusha, na hiki mlichokifanya leo ni wazi kuwa mnafanya kazi nzuri sana.

Tunaimani mchakato huu ulifuata hatua zote stahiki za kumpata Mwanamke Jembe ambaye anawakilisha  WANAWAKE  MAJEMBE wengine kutoka katika mkoa wetu, hii ni hatua nzuri ya kuwainua wanawake hawa ili na wao wafike katika  viwango vinavyohitajika katika soko la sasa la kimapinduzi katika maendeleo.

Tunawashukuru wadau wote walioshirikiana na Jembe fm katika kuifanikisha hili, Wakina mama walijitokeza hapa, wakina mama ambao wamekuwa wakijituma na kupambana katika Nyanja tofautitofauti , marafiki wote mliokuja kushuhudia utoaji wa vyeti, Tunawashukuru sana.

Na pia napenda kupitia hafla hii kuwashukuru ninyi Jembe fm, Mkurugenzi Dr Sebastian Ndege, Meneja Fred Kikoti, Mkuu wa vipindi, Kelvin Michael, Mratibu wa Mwanamke Jembe Mansour Juamnne, viongozi na watangazaji wote kwa kazi yenu nzuri mnayoifanya.

Vile vile, nawashukuru sana kwa kuiungamkono Serikali ya Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli katika jitihada za kuwaletea maendeleo Watanzania.

Nawaomba muendelee na moyo huo mwema. Namuomba Mwenyezi Mungu awaongezee pale mlipopunguza na kuendelea kuwashushia Baraka tele.

Wanawake Oyee

Serikali inatambua na kuthamini sana ushirikiano baina yenu na harakati za maendeleo katika Mkoa wetu.  

Ndiyo maana tumekuwa tunatengeneza mazingira mazuri kwa wanawake. Tumekuwa tunatoa mikopo kwa makundi ya wajasiriamali tumewaboreshea vituo Afya ,na mazingira mengine mengi
Asanteni sana kwa kunisikiliza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.