ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 24, 2018

MTOTO HUYU MLEMAVU KUSOMESHWA HADI NGAZI YA CHUO KIKUU


NA ZEPHANIA MANDIA WA GSENGO TV
TAASISI YA KIMATAIFA YA JOSEPHAT TORNNER FOUNDATION (JTF) IMEAHIDI KUMSOMESHA KUANZIA DARASA LA KWANZA, HADI CHUO KIKUU, MTOTO MWENYE ULEMAVU WA MACHO, SUNDI MASALU, KUANZIA SASA.

MKURUGENZI WA TAASISI HIYO INAYOHUSIKA NA USAIDIZI WA WATU WENYE ULEMAVU, JOSEPHAT TORNNER, AMEUHAKIKISHIA ULIMWENGU HAYO JANA, ALIPOZUNGUMZA MBELE YA WAZAZI NA VIONGOZI WA SERIKALI YA KIJIJI CHA MALILI, WILAYA YA BUSEGA MKOANI SIMIYU, MUDA MFUPI KABLA YA KUKABIDHIWA MTOTO HUYO KWENDA KUMHUDUMIA KIELIMU.

KWA UPANDE WAO, BABA NA MAMA WA WA MTOTO SUNDI, GRESS MAYALA NA MASALU BONIPHACE, WAMEUSHUKURU UONGOZI WA TAASISI YA JTF KWA UAMUZI WA KUANZA KUMSOMESHA MTOTO WAO HUYO, HUKU WAKIOMBA WALEMAVU WENGINE WAPATE MISAADA KAMA HIYO.



BAADA YA HAPO, TORNNER AKAKABIDHIWA MTOTO. SAFARI YA SUNDI YA KUVUKA MILIMA NA MABONDE IKAANZIA HAPA NYUMBANI KWAO, KUELEKEA KATIKA SHULE YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU YA BUHANGIJA, ILIYOPO MKOANI SHINYANGA.
ALIPOWAILI MKOANI SHINYANGA, SUNDI AKAPOKELEWA NA OFISA ELIMU TAALUMA WA SHULE ZA MSINGI, MANISPAA YA SHINYANGA, ESAU NYERIGA, PAMOJA NA UONGOZI WA SHULE. WAKAWA NA HAYA YA KUSEMA.
HAPA NI BUHANGIJA SHULENI KWA SUNDI. ANAANZA MAISHA MAPYA BAADA YA MIAKA TISA BILA KUIJUA ELIMU. KISHA SUNDI AKASEMA KWA LUGHA YA KISUKUMA YA BABA NA MAMA YAKE.

BAADA YA MTOTO HUYU KUKABIDHIWA TAYARI KWA KUANZA MASOMO YAKE YA DARASA LA KWANZA, KATIKA SHULE YA BUHANGIJA MKOANI SHINYANGA, TORNNER AKATOA USHAURI.

MTOTO SUNDI MASALU, MWENYE NDOTO YA KUWA NESI AU MWALIMU, AMEIBULIWA NA TAASISI YA JTF, KUPITIA KAMPENI YAKE YA PAZA SAUTI KUMLINDA MTOTO MWENYE ULEMAVU KIELIMU.

MAALIM SEIF AMUONYA LIPUMBA AMTAKA AACHE KUIVURUGA CUF.

Maali Seif amuonya Profesa Lipumba amtaka aache kukivuruga chama cha CUF Tanzania
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wanachi (CUF), Maalif  Seif Sharif  Hamad, amemkemea mwenyekiti wa chama hicho anayetambuliwa na msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania, Profesa Ibrahimu Haruna Lipumba na kumtaka kuacha kukivuruga chama hicho.
Maalim Seif amesema kuwa, muda walionao kwa sasa Wanacuf ni kwa ajili ya kukijenga chama hicho. Maalim ameyasema hayo leo wakati wa mkutano wake na wanachama wa chama hicho uliofanyika katika Hoteli ya Korini iliyopo Tandale jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine amewataka wanachama wake kuwa wamoja na kutoyumbishwa na upande wa CUF ya Lipumba.




 Profesa Lipumba, Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na msajili wa vyama vya siasa Tanzania
Amesema kwamba, Lipumba ni mtu asiye mkweli, na kuongeza kuwa, yeye ndiye aliyempokea Edward Lowassa katika Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA, hata hivyo siku chache baadaye akageuka na kudai kuwa hakubaliani na maamuzi ya kumkaribisha katika umoja huo. Mkutano baina ya Katibu mkuu wa chama hicho na wanachama hao umefanyika kwa lengo la kujenga mshikamano na umoja ndani ya chama hicho ambacho bado kinaendelea kushuhudia hali ya mchafukoge kati ya Maalim Seif na Profesa Lipumba.



Profesa Lipumba na Maalim Seif walipokuwa wakishirikiana
Katika uwanja huo, hivi karibuni Profesa Lipumba alinukuliwa akisema kuwa, chama hicho kilimdekeza kwa kiasi kikubwa Katibu mkuu wake, Maalim Seif Sharif Hamad. Kwa mujibu wa Lipumba hali hiyo imesababisha chama hicho kushindwa kupata viongozi watakaoingia katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar sambamba na kutokuwepo kwake kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK). CHANZO: Parstoday swahili.


KUHUSU TAARIFA ZA KUFUNGIA MITANDAO YA KIJAMII, SERIKALI YAFUNGUKA HAYA.

Kumekuwa na uvumi unaosambazwa katika mitandao ya kijamii kutoka kitengo cha Rais, Ikulu idara ya Mawasiliano ikidai kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imearifu wananchi wake kufungia mitandao ya kijamii nchini endapo itatumika vibaya.

Kufuatia habari hiyo ambayo hata hivyo inaonesha ni ya mwaka 2017,  Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais- Ikulu, Gerson Msigwa mapema leo hii ameikanusha barua hiyo na kudai kuwa haijachapishwa na idara yake.

Msigwa amewasihi Watanzania kuipuuza habari hiyo kwani ni uvumi ambao hauna ukweli wowote, kwani Serikali haijatoa wala kuzungumzia swala hilo.

Taarifa hii imetengenezwa na wahalifu wa mtandao. IPUUZWE. pic.twitter.com/frwWozW12U
— Gerson Msigwa (@MsigwaGerson) March 24, 2018


MAALIM AMVAA TENA LIPUMBA.


Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), Maalif  Seif Sharif  Hamad amemtolea uvivu Mwenyekiti wa Chama hicho anayeungwa mkono na Msajili wa Vyama vya siasa, Prof. Ibrahimu Lipumba akimtaka kuacha kukivuruga chama hicho kwani muda walionao kwa sasa ni kukijenga chama hicho.

Maalim ameyasema hayo leo wakati wa mkutano wake na wanachama wa chama hicho uliofanyika katika Hoteli ya Korini iliyopo Tandale jijini Dar es Salaam ambapo amewataka wanachama wake kuwa wamoja na kutoyumbishwa na upande wa Lipumba.

Amesema kuwa Lipumba ni mtu asiyekuwa mkweli, kwani yeye ndiye aliyempokea Edward Lowassa katika UKAWA lakini siku chache baadae aligeuka na kudai kuwa hakubaliani na maamuzi ya kumkaribisha katika umoja huo.

Mkutano baina ya Katibu mkuu wa chama hicho na wanachama hao ulikuwa na lengo la kujenga mshikamano na umoja ndani ya chama hicho.

CHAMA KIKUU CHA UPINZANI ZAMBIA KUMUUZULU RAIS LUNGU.

Chama kikuu cha upinzani Zambia kumuuzulu Rais Lungu





















Chama kikuu cha upinzani nchini Zambia kilmewalisha hoja bungeni kikitaka kumsaili na kumuuzulu Rais Edgar Lungu wa nchi hiyo. Chama hicho kinamtuhumu Rais Lungu kuwa amekiuka katiba. Hayo yameripotiwa leo na ofisi ya Rais wa Zambia.
Hoja hiyo iliyowasilishwa na chama kikuu cha upinzani cha UPND imesainiwa na theluthi moja ya wawakilishi wa Bunge la Zambaia lenye jumla ya wabunge 166. Ili iweze kuidhinishwa, kwa ajili ya kumsaili na kumuuzulu Rais wa Zambia, hoja hiyo inapasa kuungwa mkono na theluthi mbili ya wabunge. 
Msemaji wa Rais wa Zambia, Amos Chanda amesema kuwa huu ni mwendelezo wa jitihada zilizofeli za chama kikuu cha upinzani (UPND) za kuwasilisha hoja mahakamani kupinga ushindi wa Rais Edgar Lungu.
Hoja hiyo inatarajiwa kujadiliwa wiki ijayo tarehe 28 mwezi huu. Hoja hiyo inaeleza kuwa, Rais Lungu alikiuka katiba kwa kutokabidhi madaraka kwa Spika wa Bunge la Taifa wakati mrengo wa upinzani ulipopinga mahakamani ushindi wake mwaka 2016. Rais Lungu alichuana vikali na hasimu wake kutoka chama cha UPND, Hakainde Hichelema.


Kiongozi wa upinzani Zambia, Hakainde Hichelema  
Itakumbukwa kuwa, Rais Lungu, alimshinda Hakainde Hichilema mwaka juzi katika uchaguzi uliokuwa na ushindani mkali, lakini Hichelema alikataa kumtambua Lungu kama rais wa Zambia na kusema kura zake ziliibwa. CHANZO PARSTODAY

POLISI YATOA ONYO WANAOIBIA WATALII ZANZIBAR.


Mkuu wa Operesheni Maalum za Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi DCP Liberatus Sabas akizungumza na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Hasina Tawfiqi wakati wa Operesheni maalum ya kukabililiana na mtandao wa dawa za kulevya na uhalifu dhidi ya watalii inayoendelea katika mikoa ya Zanzibar. (Picha na Jeshi la Polisi)
Na. Jeshi la Polisi.
Jeshi la Polisi nchini limesema Operesheni ya kukabiliana na mtandao wa dawa za kulevya katika Visiwa vya Zanzibar itaendelea sambamba na kuwadhibiti wahalifu wanaofanya vitendo vya kuwaibia na kuwadhuru watalii jambo ambalo linatia doa usalama uliopo katika visiwa hivyo.

Kauli hiyo imetolewa  na Mkuu wa Operesheni maalum za Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi DCP Liberatus Sabas ambaye yupo Zanzibar akiongoza timu iliyoundwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini pamoja na Kamisheni ya Polisi Zanzibar kwa lengo la kuongeza nguvu katika kuzuia na kupambana na mtandao wa dawa za kulevya pamoja na uhalifu dhidi ya watalii.

DCP Sabas amesema Operesheni hiyo haitawaacha wahalifu hao salama kwa kuwa inafanyika kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha kuwa haiachi mhalifu yeyote anayejihusisha na vitendo hivyo viovu ambavyo vimekuwa vikichafua taswira nzuri ya usalama.

“Operesheni hii ni endelevu na niwape tu salamu wahalifu kuwa jambo la msingi ni wao wenyewe kujisalimisha kwa kuwa awamu hii hata wakikimbia tutawasaka na kuwakamata  kwa kuwa nguvu ipo na tunapata ushirikiano kwa wananchi wema wanaochukia vitendo vya uhalifu” Alisema Sabas.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja, Kamishna Msaidizi wa Polisi Hasina Tawfiqi amesema katika operesheni hiyo wamefanikiwa kukamata dawa za kulevya aina ya Heroin jumla ya Kete 695 sawa na ujazo wa gramu 31.3 pamoja na Watuhumiwa 21.

Amewasihii wakazi wa Kaskazini Unguja na mikoa jirani kuendelea kutoa taarifa ili kuweza kukomesha mtandao wa biashara hiyo pamoja na kuhakikisha kuwa watalii wanaotembelea mkoa huo wanafanya kazi zao kwa amani na usalama.
Operesheni hiyo pia imefanyika katika Mkoa wa Mjini magharibi ambapo Jumla ya watuhumiwa 58 walikamatwa pamoja na dawa za kulevya aina heroin Kete 1293 na Vifuko vitatu sawa na Gramu 74.385.

MWENYEKITI UVCCM AKUTANA NA WABUNGE WAWAKILISHI VIJANA MJINI DODOMA.

 Na zephania mandia.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Ndg. Kheri Denis James (MCC) jioni ya leo amekutana na kufanya  mazungumzo na wajumbe wanaowakilisha vijana kwa nafasi za wanawake katika vyombo vya kutunga sheria  (Wabunge  katika Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania na Baraza la wa Wawakilishi Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar) katika ukumbi wa secretariet  White house Mjini Dodoma.




Thursday, March 22, 2018

KOREA YA KUSINI YAONGOZA KUWA NA WAFANYAKAZI WAPENDA KAZI KUPITA KIASI.


Serikali nchini Korea Kusini imeanzisha mpango wa kuwalazimisha wafanyakazi kuondoka kwa wakati baada ya kumalizika kwa zamu yao.

Mpango huo unahusisha kuzimwa kwa lazima kwa kompyuta za wafanyakazi hao afisini saa mbili usiku kila Ijumaa.

Lengo la mpango huo ni kujaribu kufikisha kikomo "utamaduni wa kufanyakazi muda wa ziada".

Wafanyakazi nchini humo hufanya kazi muda mwingi zaidi kwa siku ukilinganisha na wafanyakazi wengine nchi nyingine duniani.

Wafanyakazi wa serikali Korea Kusini kwa kawaida hufanya kazi saa 2,739, muda ambao ni saa 1,000 zaidi ya muda wanaofanya kazi watumishi wa umma katika mataifa yaliyoendelea.

Mpango huo wa kuzima kompyuta kwa lazima utaanza kutekelezwa na serikali ya jiji la Seoul kwa awamu tatu katika kipindi cha miezi mitatu ijayo.

Utaanza kutekelezwa mnamo 30 Machi, ambapo kompyuta zote zitakuwa zinazimwa saa mbili usiku.

Awamu ya pili itaanza Aprili kwa kompyuta kuzimwa saa moja unusu usiku Ijumaa ya pili na ya nne ya mwezi.

Kuanzia Mei, mpango huo utaanza kutekelezwa kikamilifu ambapo kila Ijumaa saa moja jioni kompyuta zitakuwa zinazimwa kwa lazima.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa serikali ya jiji la Seoul, wafanyakazi wote wataathiriwa na mpango huo, ingawa baadhi wanaweza kuepushwa kukiwa na hitaji maalum.

Hata hivyo, si wafanyakazi wote wanaofurahia mpango huo.

Serikali hiyo inasema 67.1% ya wafanyakazi wa serikali wameomba kutoshirikishwa kwenye mpango huo.

Mapema mwezi huu, bunge la Korea Kusini lilipitisha sheria kupunguza saa za kufanya kazi kila wiki kutoka saa 52 hadi saa 68.

Katika mataifa mengi, watu hufanya kazi saa 40 kwa wiki.

KAMPUNI ILIYOTAKA KUIPIGA TANZANIA KWENYE E- PASSPORT, YAVUNJIWA MKATABA NA SERIKALI YA UINGEREZA

Muonekanao wa E-Passport zilizotolewa mapema mwaka huu.

Passport ya Uingereza ambayo kampuni ya De La Rue ilikuwa inazitenegeneza kabla ya kufutiwa mkataba wao.

*Ni ile iliyonyimwa zabuni ya kutengeneza hati mpya za kusafiria Tanzania
*Uingereza nayo yaamua kuvunja nayo mkataba kutokana na gharama kubwa
*Uongozi wa kampuni wachanganyiwa, hisa zao zashuka kwa kasi soko la hisa
Na Mwandishi wetu

KAMPUNI ya De La Rue ambayo ilishindwa kwenye zabuni ya E-Imigration ambapo ingetengeneza e-passport, e-Visa, e-Imigration nchini Tanzania imepata pigo jingine baada ya mkataba wake kusitishwa na Serikali ya Uingereza ya kuendelea kutengeza hati za nchi hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Aliance News imesema kuwa kampuni ya De La Rue ilikuwa na mkataba na Uigereza wa miaka 10 lakini nchini hiyo imeamua kuvunja mkataba kati yake na kampuni hiyo.

Imefahamika lengo la Serikali ya Uingereza kuvunja mkataba huo wa kutengenezwa hati za kusafiria ni kutokana na gharama kuwa kubwa za utengenezaji wa hati hizo na hivyo kuamua kuipa zabuni kampuni ya French firm Gemalto.

"Hati mpya za kusafiria za Uingereza hazitatengenezwa tena na kampuni ya De La Rue ambayo ndio iliyotengeneza hati zitumikazo kwa sasa.

"Hivyo hati hizo mpya za rangi ya blue ambazo zitatumika baada ya Uingereza kujitoa katika Umoja wa Ulaya zitatengenezwa na kampuni ya French firm Gemalto. Kubadilika kwa rangi ya hati hiyo kunatafsiriwa kuwa ni alama ya kurudi kwa nguvu ya Uingereza, umesema mtandao ulitoa taarifa hizi.

Pia taarifa zinaeleza kuwa Kampuni ya De La Rue inafikiria kukata rufaa baada ya kukosa na kushindwa katika zabuni ya kutengeneza hati hizo mpya.

Kampuni hiyo imeripotiwa ikidai haikuridhishwa kwa kupoteza zabuni hivyo hivyo inaweza kukata rufaa kutokana na uamuzi huo wa Serikali ya Uingereza

Hata hivyo Mkurugenzi wa Fedha wa kampuni ya De La Rue Jitesh Sodha amesema kitendo hicho kimesababisha hisa za kampuni yao kutoka asilimia 14 ya Jumanne ya wiki hii hadi kufikia asilimia 0.4 leo Machi 22 ya mwaka huu.

"Tumechukizwa na kitendo cha Serikali ya Uingereza kusitisha mkataba wetu wa kutengeneza hati za kusafiria za nchi hiyo wa miaka 10 kwani ulikuwa mkataba unamalizika Julai mwakani.

Hivi karibuni katika uzinduzi wa E-Passport, Rais Dk. John Magufuli amesema kuwa kuna wajanja awali walipanga kuutekeleza mradi huo kwa gharama kubwa kiasi cha dola za kimarekani milioni 226 ambazo ukizibadili kwa Dola moja sawa na shilingi 2245 mradi huo ungegharimu shilingi za kitanzania bilioni 507.

Rais Magufuli alisema baada ya kugundua ujanja huo Rais alivituma vyombo vya dola kufuatilia na kubainika mradi huo unaweza kutekelezeka kwa gharama nafuu na za kawaida ambapo baadae mradi umeonyesha kutelekezwa kwa dola milioni 57.8 sawa na bilioni 129 za kitanzania na hivyo kuliokolea taifa upotevu ambao ungeweza kujitokeza wa zaidi ya shilingi bilioni 380.

Moja ya kampuni ambayo ilikosa zabuni ya kutengeneza hati mpya ya kusafiria nchini Tanzania ni hiyo ya De La Rue na moja ya sababu ilikuwa ni kiasi kikubwa cha fedha ambazo walikihitaji lakini Serikali iliwashutukia na kuamua kutoa zabuni kwa kampuni nyingine iliyotengeza kwa gharama nafuu.

Hata hivyo vyanzo vya kuaminika kutoka Serikali ya Tanzania vilibanini mambo mazito yaliyoibuka baada ya kubainika kampuni hiyo kuhonga mamilioni ya fedha ili kuichafua mradi wa hati za kusafiria na uhamiaji kwa ujumla.

COCA COLA YAJA NA PROMOSHENI YA 'MZUKA WA SOKA NA COKA'

 Maofisa wa kampuni ya Coca-Cola mkoani Mwanza, kutoka kushoto Meneja Mauzo Mkoa , Mnyamuhanga Gavana,Meneja Mauzo na Masoko Samuel Makenge na Meneja Mauzo Mwandamizi Deus Kadico, wakionyesha mfano wa chupa zenye vizibo vyenye zawadi ya promosheni ya ‘Mzuka wa Soka na CoKa’ iliyozunduliwa jijini humo.
Meneja Mauzo na Masoko wa kampuni ya soda ya Cocacola tawi la Mwanza Samuel Makenge, akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza wakati wa uzinduzi wa promosheni.

* Lengo ni kuwezesha wapenzi wa soka kupata burudani ya Kombe la Dunia 2018

Wakati michuano ya Kombe la Dunia 2018, ambayo mdhamini wake mkuu ni kampuni ya Coca-Cola inakaribia kuanza,kampuni ya kutengeneza vinywaji ya Nyanza Bottlers leo imezindua promosheni itakayotoa fursa kwa wateja wake kujishindia luninga za kisasa, zitakazowezesha kufaidi uhondo wa michuano ya kombe la dunia wakiwa majumbani kwao.

Promosheni hii ambayo inajulikana kama ‘ Mzuka wa Soka na CoKa’ itawahusu watumiaji wa soda za Coca-Cola, Sprite, Fanta, Sparleta na Stoney Tangawizi katika mikoa ya Kanda ya ziwa .

Mbali na zawadi za televisheni,watumiaji wa vinywaji vya kampuni ya Coca-Cola, kupitia promoheni hii wataweza kujishindia zawadi nyinginezo mbalimbali ikiwemo ,fedha taslimu kati ya shilingi 5,000 mpaka shilingi 100,000/-kofia, t shirt,soda za bure na zawadi kubwa ya bodaboda.

Meneja Masoko na Mauzo wa kampuni ya Nyanza Bottlers,Samwel Makenge ,amesema Coca-Cola ikiwa ni mdhamini mkuu wa mashindano ya Kombe la Dunia 2018,imekuja na promosheni ya kuleta shangwe za mashindano hayo katika mkoa wa Mwanza,utakaowawezesha wateja wake kufurahia mashindano haya ya soka makubwa duniani wakati huohuo wakiburudika na vinywaji vya Coca-Cola na kujishindia zawadi kemkem.

“Wakati michuano ya Kombe la Dunia inakaribia kuanza,tumeona tuje na promosheni hii ambayo itawezesha watumiaji wengi wa vinywaji vya kampuni yetu kujisindia luninga za kisasa aina ya SONY LED zenye kioo cha mbele bapa ili wapate uhondo wa mashindano hayo.Kinachotakiwa ni kunywa soda na kushinda zawadi”.Alisema Makenge.

Mkuu wa Masoko na Mauzo wa Nyanza Bottler,Japhet Kisusi,alisema ili kujishindia zawadi anachotakiwa kufanya mtumiaji wa soda ni kuangalia ganda la chini ya kizibo baada ya kunywa soda linakuwa na picha ya zawadi aliyobahatika kujishindia. “Kwa upande wa zawadi ya pikipiki anachotakiwa kufanya mteja ni kuunganisha picha tatu vinavyokamilisha picha ya pikipiki kutokana na ganda atakalokuta ndani ya soda.kuna sehemu ya mbele,kati na nyuma.Zawadi zote kubwa zitachukuliwa kiwandani na ndogo kama kofia,T shirt na soda za bure zitatolewa na mawakala wa kampuni waliosambaa maeneo mbalimbali”.Alisisitiza.

Kwa upande wake,Meneja wa Chapa ya Coca-Cola nchini,Sialouise Shayo,alisema promosheni hii inadhihirisha dhamira ya kampuni ya kuwawezesha wateja wake na watanzania kwa ujumla kupata 'Mzuka wa Soka na Coka' katika msimu wa kombe la Dunia na kujisikia sehemu ni sehemu ya mashindano hayo.

Katika maandalizi ya Mashindano ya Kombe la Dunia 2018,Coca-Cola imetangaza hivi karibuni kuwa msanii mmoja wa Tanzania atashirikiana na mwanamziki nguli wa kimataifa, Jason Derulo ,kutengeza wimbo maalumu wa mashindano hayo wenye vionjo vya Tanzania.

KARIBU TANZANIA, KARIBU BUJORA CULTURAL CENTRE.



Bujora Cutural Centre ni kitengo cha Kutoa elimu, Historia na Tamaduni za Asili ya Wasukuma kinacho patikana ndani ya kituo cha Makumbusho ya watu wa kabila hilo kilichopo Kisesa mkoani Mwanza.

Kituo hiki kimebarikiwa kuwa na hazina kubwa ya kumbukumbu za asili na sanaa zilizohifadhiwa bila kufutika na hata hii leo zikatumika kuwa kielelezo kwa vizazi na vizazi.

Utamaduni wa Wasukuma umetanda maeneo mengi nchini Tanzania, kama ilivyo kwa wingi wa idadi ya watu wa kabila hilo vivyo hivyo tamaduni zao zimeenea kutanda na kujulikana kila mahali.

Ukisema wapi Usukumani, bila shaka moyo wa watu wa kabila hilo umejikita Kanda ya Ziwa kwa mikoa ya Mwanza, Shinyanga na kwa nafasi fulani mkoani Mara maeneo ambayo yanamizizi ya kutosha ya watu wa asili hiyo.
...............................................................................................................................................
The Bujora Cultural Centre and Sukuma Museum in Kisesa, are historical institutions founded for the education and support of Sukuma culture. The arts of the Sukuma culture are among the richest in East Africa.

As the Sukuma people are the largest cultural group in Tanzania, the Sukuma culture is dispersed throughout the country.

The heart of Usukuma is in the Lake Zone of Mwanza, Shinyanga and the Mara regions where the legacy of a rich art tradition is now maintained.

MMILIKI WA FACEBOOL AWAOMBA RADHI WATUMIAJI WA MTANDAO WAKE.

Mkurugenzi Mkuu na mmliki wa mtandao wa kijamii wa Facebook Mark Zuckerberg amevunja ukimya juma hili kuhusu kashfa iliyoikumba kampuni yake ambapo ameomba radhi kutokana na "kuvunja uaminifu" kwa weteja wake zaidi ya bilioni moja na kuapa kutorudia makosa yaliyojitokeza.
Katika matamshi yake ya kwanza kwa umma kuhusiana na matumizi mabaya ya taarifa binafsi za wateja zaidi ya milioni 50 kulikofanywa na kampuni ya Uingereza iliyokuwa na uhusiano na timu ya kampeni ya Rais Donald Trump mwaka 2016, Zuckerberg amewaambia watumiaji wa Facebook kuwa taasisi yake "ilikuwa na wajibu wa kulinda taarifa zao."
Ameahidi pia kuwa Facebook itachunguza kila programu iliyopata mwanya wa kupitia akaunti za wateja wake na kufanya uchunguzi wa kisayansi kwa kitu chochote kilichoonekana kina wasiwasi.
"Huu ulikuwa ni uvunjifu mkubwa wa matumizi ya taarifa binafsi na uaminifu, nawaomba msamaha kwa kile kilichotokea," alisema Zuckerberg wakati akihojiwa na kituo cha televisheni cha CNN.
Imebainika kuwa kampuni ya Uingereza Cambridge Analytica ilifanikiwa kudukua taarifa binafsi za mamilioni ya watumiaji wa mtandao wa kijamii wa Facbook kupitia progarmu maalumu ya utafiti uliofanywa na Aleksander Kogan na ambayo ilipakuliwa na mamilioni ya watumiaji wa mtandao huo na kuchukua taarifa za marafiki wengine.
"Hiki kilikuwa kitendo cha uvunjifu wa uaminifu kati ya Kogan, Cambridge Analytica na Facebook," aliandika Zuckerberg. "Lakini ni kuvunja uaminifu kati ya Facebook na watu ambao wametoa taarifa zao kwetu na walitarajia tuzilinde."

TAASISI YA KIMATAIFA YAPAZA SAUTI ELIMU KWA WATU WENYE ULEMAVU NCHINI


​NA ZEPHANIA WA GSENGO TV 
SERIKALI imeshauriwa kuondoa vikwazo vya kielimu, kwa watu wenye ulemavu nchini, ili kusaidia jamii hiyo kufikia malengo yao ya kiuchumi.

Kauli hiyo imetolewa na mkurugenzi wa Taasisi ya Kimataifa, ya Josephat Tornner Foundation (JTF), katika SIKU YA KUPAZA SAUTI kuwalinda watoto wenye ulemavu duniani, iliyofanyika wilayani Busega, mkoa wa Simiyu.
Maadhimisho hayo yaliyotanguliwa na maandamano ya wanafunzi, kisha baada ya kutimu saa 5:00 asubihi, Kengele ya kupaza sauti kuungana na mataifa zaidi ya 40, ikapigwa.

Mkuu wa wilaya ya Busega, mkoa wa Simiyu, Tano Mwera naye akatoa maagizo ya Serikali.

Kwa upande wake, Baba mzazi wa mtoto Sundi Masalu, Masalu Boniphace, ambaye tangu mwanaye azaliwe miaka tisa iliyopita hajawahi kupelekwa shuleni.
.
MAADHIMISHO YA KUPAZA SAUTI KUMLINDA MTOTO MWENYE ULEMAVU, HUFANYIKA MACHI 21 KILA MWAKA DUNIANI KOTE, AMBAPO WILAYA YA BUSEGA IMETAJWA KUWA NA WANAFUNZI 223 WENYE ULEMAVU WA AINA MBALIMBALI.














Wednesday, March 21, 2018

HAYA HAPA MAGOLI YOTE VIJANA WA TANZANIA U20 WAKIICHAPA MSUMBIJI 2-1


Timu ya Taifa ya Vijana wenye umri chini ya miaka 20 ‘Ngorongoro Heroes’ leo imeichapa timu ya vijana wenye umri huo ya Msumbiji mabao 2-1 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliopigwa katika dimba la Taifa, jijini Dar es Salaam. Tazama hapa mabao yote yaliyofungwa kwenye mchezo huo, huku vijana wa Tanzania wakikosa penati.

RAIS WA MYNMAR AJIUZULU.


Rais wa Myanmar Htin Kyaw amejiuzulu, kulingana na afisi yake.

Hakuna sababu ilitolewa lakini kumekuwa na wasiwasi katika miezi ya hivi karibuni kuhusu afya ya rais huyo mwenye umri wa miaka 71 baada ya kuonekana amedhoofika katika hafla moja.

Htin Kyaw alliapishwa kuwa rais 2016 baada ya uchaguzi uliositisha miongo kadhaa ya uongozi wa kijeshi.

Lakini alikuwa kiongozi asiye na mamlaka huku aliyekuwa kiongozi wa upinzani wa muda mrefu Aung San Suu Kyi akiwa kiongozi mwenye mamlaka.

Taarifa iliochapishwa katika mtandao wa facebook wa rais huyo ilisema kuwa Htin alitaka kupumzika.

Makamu wa rais Myint Swe , jenerali wa zamani atakuwa kaimu rais hadi pale rais mpya atakapochaguliwa katika muda wa siku saba sijazo, taarifa hiyo ilisema.

Bi Suu Kyi, ambaye alifungwa kwa miaka kadhaa chini ya uongozi wa kijeshi wa Junta alipigwa marufuku kuchukua wadhfa huo.

Kipengee cha katiba kilichotengezwa ili kuhakikisha achukui wadhfa huo kinasema kuwa hakuna raia mwenye watoto kutoka nje anaweza kuwa rais.

Alikuwa na watoto wawili na mumewe raia wa Uingereza.

Htin Kyaw alikuwa rafikiye wa utotoni na mshauri wake wa zamnai na wakati mwengine dereva. Alionekana kuwa mtulivu na mtu alimuamini sana.

HATIMAYE ABDUL NONDO AMEFIKISHWA MAHAKAMANI MKOANI IRINGA

Hatimaye Abdul Nondo amefikishwa Mahakamani Iringa Tanzania
Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo amesafirishwa usiku wa kuamkia leo Machi 21, 2018 kupelekwa mkoani Iringa.
Taarifa zilizotolewa na wakili wake, Jebra Kambole leo Jumatano zinaeleza kuwa sasa Nondo yupo Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa.
Nondo anadaiwa kutoweka katika mazingira ya kutatanisha Machi 6, 2018 na siku inayofuata akaonekana mjini Mafinga, wilayani Mufindi, Iringa ambako alishikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo na baadaye kurejeshwa Dar es Salaam.
Tangu akamatwe Nondo hajawahi kuzungumza na wakili wake wala mtu yeyote wa karibu yake jambo ambalo limekuwa likipingwa na watetezi wa haki za binadamu.
Jana, Jebra alisema kuwa wamefungua kesi ya kuiomba mahakama kumpa dhamana Nondo, kutoa amri ya kuwapa mawakili haki ya kuonana naye na kuitaka mahakama itamke mwanafunzi huyo wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) ameshtakiwa kinyume cha sheria.
Kumekuwepo kesi kadhaa za kutoweka watu hususan wanasiasa nchini Tanzania suala ambalo limezusha wasiwasi kuhusu utendaji wa Jeshi la Polisi na vyombo vya usalama nchini humo.

BARUA YA WAZI KWA NAIBU WAZIRI WA HABARI UTAMADUNI VIJANA NA MICHEZO KUTOKA WASAFI.


Muheshimiwa Salaam,
Natumai u mzima wa afya.

Najua una nia nzuri ya kulinda maadili y amwafrika na hasa ya mtanzania na kuhakikisha basi hakuna ovu lolote linaloweza kuichafua sifa yetu lakini kubwa jamii zetu. Ila naomba nisahihishe approach yako.

Muheshimiwa kuna vitu vinaitwa Ratings nadhani huu ni Muda muafaka kwa tasnia yetu kuanza kua na hii system ili basi wasanii wafanye kazi kwa uhuru na pia hadhira (watazamaji na waskilizaji) pia wasipitwe ama kukosa kazi za wasanii wanaowapenda
Mfano wa ratings ni G ikiwa inamaanisha General yaani yeyote anaweza kutazama
PG hii inaweza tazamwa na yeyote ila watoto wanahitaji usimamizi wa wazazi kwani kuna baadhi ya material sio kwa ajili yao PG-13 wazazi wanahitajika, ikiwezekana aitazame movie, video yote kwanza kabla ya kumuonesha mtoto Na zingine kibao.
Hii ni 2018 sio mwaka 1903 sasa ivi tunachotakiwa kufanya ni kuanza kutambulisha hii system na sio kufungia nyimbo. 

Lakini mbali na hayo, badala ya kushusha na kuzuia wasaniii kama kina @diamondplatnumz na wengine mlofungia kazi zao embu tazameni Tasnia nzima kwa ujumla. 

Kuna watu wanatamani sana kuingia katika sanaa wakiwa na vipaji na uwezo ila wakiangalia yanayowakuta malegend kama kina majuto wanakata tamaa. Huwezi nambia mzee kama majuto leo na movie zote alizoekt hakuna kitu tasnia imeweza kumfanyia na yeye aishi kama hadhi ya jina lake.

Si majuto tuu wako wasanii wengi sana ambao wananafasi kubwa katika kuelimisha jamii lakini maisha wanayoishi ni tofauti na status zao. Je sanaa sasa ni kulinda maadili tu ama ni ajira pia? 

Kazi za wasanii zinasimamiwa ipasavyo?

Je! Mnahakikisha kwamba wasanii hawanyonywi na mapromota?
Mnahakikisha kwamba hakuna watu ambao wao ndo wanajifanya Miungu wa kuwatawala wasanii na kuwanyonya wanaokataa kuwaabudu?

Ama wewe unaona kuzuia kazi ndo la msingi?

Unajua kwamba @diamondplatnumz ni msanii wa kimataifa kutoka Tanzania? 

Unataka afate maadili ya kitanzania Jeh! Mashabiki zake wa nje nao kama wamarekani wanaishi maadili ya kitanzania? Kiti umepewa sio ulemaze sanaa yetu irudi nyuma, ivushe ifike mbali. 

Badili sana yetu iwe accessible kimataifa sio kuiwekea mipaka.

Ni hayo tu Muheshimiwa naibu Waziri
Salaam kwako.

Tuesday, March 20, 2018

MNEC MWAKA RAMADHAN AMEVUNA WANACHAMA WAPYA (80) KATA YA MKWAWA MANISPAA YA IRINGA

 Mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (CCM) Taifa na mjumbe wa kamati utekelezaji wa UWT taifa Mwaka Ramadhan akiongea na wanawake waliokuwa wamejitokeza kumsikiliza kwenye ziara ya UWT taifa mkoani Iringa katika Kata ya Mkwawa
Baadhi ya wanachama waliojiunga na umoja wa wanawake UWT katika kata ya Mkwawa wakatika wa ziara ya viongozi wa kitaifa mkoani Iringa
Baadhi ya wanachama wa chama cha mapinduzi wakiwa katika kitendo cha kula kiapo pamoja na wanachama waliojiunga na umoja wa wanawake UWT kata ya Mkwawa
 Mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (CCM) Taifa na mjumbe wa kamati utekelezaji wa UWT taifa Mwaka Ramadhan akiwa na mbunge wa viti maalum Ritta Kabati pamoja na mwenyekiti wa UWT manispaa ya Iringa Ashura Jongo Pamoja katibu wa UWT manispaa ya Iringa


Na Fredy Mgunda,Iringa

MJUMBE wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (CCM) Taifa na mjumbe wa kamati utekelezaji wa UWT taifa Mwaka Ramadhan amevuna wanachama wapya zaidi ya themanini (80) katika kata ya Mkwawa Manispaa ya Iringa ambo wamejiunga rasmi na umoja huo.

Wanachama hao wamepokelewa wakati wa ziara ya viongozi wa ngazi za juu wa UWT taifa mkoani Iringa, ambapo MNEC Ramadhan alipokuwa akiongea na wanachama pamoja na wananchi wa kata ya Mkwawa ndipo waliposhawishika kujiunga na umoja huo kutokana na hamasa walioipata kutoka kwa MNEC huyo.

Ramadhan alisema kuwa chama cha mapinduzi ni chama ambacho kimejengwa kimisingi ya kulea jumuhia  mbalimbali ambazo zipo ndani ya chama hicho ndio maana bado kinanguvu katika siasa za hapa nchini hata kimekuwa mfano kwa nchi nyingine.

“Jumuiya ya umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi Tanzania ni moja kati ya jumuiya ambayo ipo ndani ya chama hiki na inakazi zake kwa ajili ya kukijenga chama na kuleta maendeleo kwa wananchi waliokipa dhamana ya kuongoza nchi hii” alisema Ramadhan

Aidha Ramadhan aliwataka wanawake kujifunza kujifunza kujitegemea ili waweze kuja kuwaajiri wanaume ambao kwa sasa ndio wamekuwa wakitoa ajira nyingi kwa wanawake hapa nchini.

“Wanawake wenzangu sasa imefika mwisho wa kuwa tegemezi kwa wanaume inatakiwa sasa tusimame sisi kama sisi na tuanze kuwaajiri na kulisha wanaume zenu majumbani kwetu maana tunauwezo wa kufanya kila kazi hizo inatakiwa tujitume” alisema Ramadhan

Ramadhan alisema kuwa wanawake mkiwa mnataka kufanya biashara zenye malengo msiogope kwenda kukopa maana siku hizi kuna mikopo ya bei rahisi na riba yake sio kubwa ambayo itakuwezesha kufanya biashara yako kwa maendeleo yako.

“Siku hizi kuna mabenk mengi yanawakopesha wanawake na wanawaamini sana wanawake kwenye kufanya biasha hivyo nendeni mkakope msiogope maana hizi benk zipo kwa ajiri ya kusaidia kuinua maisha ya mtanzania” alisema Ramadhan

Ramadhan alimalizia kwa kuwataka wanawake wa kata ya Mkwawa mkoani Iringa kuzitumia pesa kwa nidhamu ya hali ya juu ili ziweze kuleta matunda ya kuleta maendeleo ambayo yanahitajika kwa maisha yao.

“Jamani kila pesa ukiitumia kwa nidhamu basi utaona faida yake na itakuletea maendeleo yako na taifa kwa ujumla maana unakuwa umetumia vizuri pesa kwa maendeleo” alisema Ramadhan

Kwa upande wake mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati alisema kuwa atawapatia elimu ya ujasiliamali ili wakipata mitaji waweze kuitumia vizuri kwa ajili ya manufaa ya maendeleo.

“Jamani mimi nimekuwa nikitoa elimu ya ujasiliamali mara kwa mara kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kufanya biashara zenu kwa faida na kutoa elimu ya matumizi ya fedha hivyo nawaomba nikiitisha tena kutoa elimu mkaribia kwa wingi maana huwa inakuwa bure” alisema Kabati